TAARIFA MPYA

Madhara ya Chai na Kahawa Kiafya

Picha
CAFFEINA/KAFEINA. Kafeina ni nini?: 1. Kafeina ni madawa ya kulevya kundi la ‘Stimulants drugs’. Utashangaa. Habari ndiyo hiyo. Hii ndiyo sababu kwa mtu aliyezoea kunywa chai hii kila siku au kahawa, siku asipokunywa kichwa humuuma, ni kwa sababu amekuwa mtegemezi au teja wa kafeina. Kafeina ni kiungo mhimu karibu katika soda zote zenye rangi nyeusi; Coca-cola, Pepsi, Sayona nyeusi, Azam cola na kadharika. Kafeina huongezwa pia katika Red bull, Malta na katika baadhi ya dawa za kupunguza maumivu mwilini. Kwahiyo Kafeina ambayo hupatikana katika chai na kahawa ni aina mojawapo ya madawa ya kulevya. 2. Kafeina ni kikojoshi (diuretics). Kafeina ni dawa ya kukufanya ukojowe. Ukinywa kikombe kimoja cha kinywaji chenye kafeina yaani chai au kahawa, basi muda si mrefu utaenda kukojoa vikombe viwili. Kwa sababu kafeina ni taka isiyotakiwa mwilini, mwili utafanya kila uwezalo ikibidi ujikamuwe wenyewe kupata maji ya ziada kuweza kuitoa kafeina hii uliyoinywa kwa kisingizio ch...

ZITTO KABWE AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA UKAWA

Dar es Salaam. Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa juu wa vyama vinavyoundwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Viongozi waliofanya mazungumzo na mbunge huyo wa Kigoma Mjini ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe; Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia pamoja na Mwenyekiti wa Chaumma, Hashim Rungwe ambaye hivi katibuni alialikwa Ukawa kujadili kasoro za uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika hivi karibuni. Ukawa inaundwa na vyama vya Chadema, NLD, CUF na NCCR-Mageuzi na vyote vimetangaza kutoshiriki uchaguzi mdogo wa ubunge utakaofanyika Januari 13, 2018.

Katika taarifa yake, Zitto alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuagizwa na uongozi wa Taifa wa ACT-Wazalendo uliomtaka kuwafikia wadau wote wa demokrasia na kuweka mikakati ya pamoja.

“Uongozi wa Taifa wa ACT-Wazalendo umeanzisha mazungumzo na vyama vyote vya upinzani nchini ili kuona njia bora zaidi ya mapambano ya pamoja ya kukabiliana na vitendo vinavyofanywa na chama tawala vya kuvuruga chaguzi huru na za haki,” alisema Zitto.

Mwanasiasa huyo alisema wakati Katibu Mkuu wa chama hicho, Dorothy Semu akiendelea na utaratibu rasmi wa kutekeleza jambo hilo, yeye alipewa wajibu wa kuanzisha mazungumzo na viongozi wa juu wa Ukawa.

“Jana (juzi), nimezungumza na Mbatia aliye hospitalini KCMC–Moshi baada ya ajali, namuomba Mola ampe afya njema. Pia nilikutana na Mbowe na nina furaha mazungumzo yetu yameanza vizuri,” alisema Zitto ambaye aliwahi kuwa naibu katibu mkuu wa Chadema kabla ya kuondoka na kuanzisha ACT-Wazalendo.

Kiongozi huyo pia alikutana na Rungwe na kufanya naye mazungumzo.

“Mazungumzo yetu yatazalisha jambo zuri kwa Taifa,” aliongeza kiongozi huyo.

Hatua hiyo ya Zitto imekuja baada ya kupita siku chache kwa viongozi wa Ukawa kutoa tamko la kuitaka NEC kuahirisha uchaguzi wa marudio wa ubunge katika majimbo matatu na udiwani wa kata sita uliopangwa kufanyika Januari 13, ili kuruhusu majadaliano.

Viongozi hao wa Ukawa, wakiongozwa na Mbowe walisema majadialiano hayo yatalenga kujadili kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi wa marudio katika kata 43, vinginevyo hawashiriki uchaguzi wa Januari.

Maoni

ZILIZO SOMWA MARA NYINGI

ULAJI WA MARA KWA MARA WA MBEGU ZA MABOGA HUKUKINGA NA KUKUEPUSHA NA MAGONJWA 1O MWILINI MWAKO...

Dalili 6 zitakazokuonyesha kuwa mwenzi wako ana mtu mwingine katika mahusiano

FAIDA YA JUICE YA KAROTI KATIKA MWILI WA BINADAM

DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO

AINA ZA MBOLEA & MATUMIZI YAKE KITAALAM

Madhara ya Chai na Kahawa Kiafya

Fahamu Aina 7 Za Juisi Zenye Kuondoa Sumu Mwilini

Ugonjwa wa Chango La Uzazi

Madhara Ya Kuangalia Video za Porno {Ngono} na Namna ya Kujizuia

Athari za kiafya za vyakula vyenye Wanga