TAARIFA MPYA

Madhara ya Chai na Kahawa Kiafya

Picha
CAFFEINA/KAFEINA. Kafeina ni nini?: 1. Kafeina ni madawa ya kulevya kundi la ‘Stimulants drugs’. Utashangaa. Habari ndiyo hiyo. Hii ndiyo sababu kwa mtu aliyezoea kunywa chai hii kila siku au kahawa, siku asipokunywa kichwa humuuma, ni kwa sababu amekuwa mtegemezi au teja wa kafeina. Kafeina ni kiungo mhimu karibu katika soda zote zenye rangi nyeusi; Coca-cola, Pepsi, Sayona nyeusi, Azam cola na kadharika. Kafeina huongezwa pia katika Red bull, Malta na katika baadhi ya dawa za kupunguza maumivu mwilini. Kwahiyo Kafeina ambayo hupatikana katika chai na kahawa ni aina mojawapo ya madawa ya kulevya. 2. Kafeina ni kikojoshi (diuretics). Kafeina ni dawa ya kukufanya ukojowe. Ukinywa kikombe kimoja cha kinywaji chenye kafeina yaani chai au kahawa, basi muda si mrefu utaenda kukojoa vikombe viwili. Kwa sababu kafeina ni taka isiyotakiwa mwilini, mwili utafanya kila uwezalo ikibidi ujikamuwe wenyewe kupata maji ya ziada kuweza kuitoa kafeina hii uliyoinywa kwa kisingizio ch...

Kauli ya ACT-Wazalendo baada ya Zitto Kabwe Kukutana na Viongozi wa Upinzani

Baada ya kuenea kwa picha za Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kuwa na baadhi ya viongozi wengine wa vyama vya upinzani hatimae chama hicho kimeeleza kuwa kiliazimia kuanza kufanya mazungumzo na viongozi wengine wa vyama vya upinzani ili kuunganisha nguvu kwenye mapambano ya demokrasia.

Akiongea na Bongo5 leo, Katibu Itikadi na Uenezi wa Chama hicho, Ndugu.Ado Shaibu amesema kuwa ingawa kila Chama kina Itikadi, sera na programu zake, yapo mambo ambayo Chama cha upinzani hakiwezi kufanya peke yake.

“Kamati Kuu ya Chama chetu iliazimia kuwa Uongozi wa juu wa Chama uanze mazungumzo na viongozi wengine wa Vyama vya upinzani ili kuunganisha nguvu kwenye mapambano ya demokrasia. Ingawa kila Chama kina Itikadi, sera na programu zake, yapo mambo ambayo Chama cha upinzani hakiwezi kufanya peke yake. Moja ya mambo hayo ni mapambano ya kidemokrasia kwa hiyo, Zitto amekwishafanya mazungumzo na Mbowe na Rungwe na atafanya mazungumzo na viongozi wa Vyama vingine,” amesema Ado.

Maoni